Maisha amefika Darasa la Saba. Amekua kimwili na akili imepevuka kiasi. Ameanza kujitadhimini na kutambua mazingira tofauti yanayomzunguka Pamoja na changamoto zake. Maisha amegundua kwamba wazazi ni wazito katika kuongea masuala ya ngono na vijana wao. Hali hii imewaweka vijana njia panda, huku jamii ikiwa inajiundia ngao ya ukimya kuhusu masuala nyeti kama haya. Vijana wanapaswa wafanye nini ili kuwafanya wazazi wachukue wajibu wa kuwaokoa vijana wao? Je, Maisha amejizatiti vya kutosha kukabili changamoto hizi? Kujithamini kutamfaa vipi ?.